Nyota wa muziki wa Pop Madonna ameanguka jukwaani wakati akitumbuiza shoo yake kwenye tuzo za Brit 2015.
Mwanamuziki huyo aliteleza kwenye
ngazi na kuanguka kwa mgongo ikiwa ni mwanzo wa shoo wakati wakati
dansa wake akijaribu kumvua joho alilovaa.
Hata hivyo mwanamuziki huyo
alionyesha ukomavu katika gemu baada ya kuugulia maumivu na kuendelea
na kumalizia wimbo wake wa Living For Love, aliokuwa akiuimba.
Baadae Madonna ametoa taarifa kuwa
yupo salama, na joho lililopelekea kuanguka kwake limefungwa imara.
Anguko lake lilianza hivi
Hapa akizidi kwenda chini
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni