Mwanamuziki wa muziki wa kizazi
kipya nchini Tanzania Rashidi Abdallah Makwaro Maarufu kama 'Chid
Benz' leo amehukumiwa kifungo cha miaka mwili jela au kulipa faini ya
shingili laki tisa.
Hukumu hiyo imetolewa leo katika
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya kupatikana na hatia ya
makosa matatu ikiwemo kukutwa na dawa za kulevya aina ya heroin yenye
thamani ya sh. 38,638, bangi yenye tahamani ya sh. 1,720 na vifaa ya
kuvutia dawa hizo kijiko na kigae.
Awali Februari 18 Chidi Benz alikiri
mbele ya Hakimu Mkazi, Waliarwande Lema mashtaka matatu yanayomabili
katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ya kukutwa na dawa za kulevya,
kifuu cha nazi na kijiko vinavyotumika kuvutia ama kunusa dawa hizo
za kulevya.
Rapa huyo amefanikiwa kulipa faini
hiyo ya shilingi laki 9, na kuachiwa huru baada ya mama yake mzazi
kuilipa.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni