Ubalozi wa Marekani nchini Uganda
umetoa tahadhari ya dharura kwa raia wake nchini Uganda hapo jana
inayosema kuwa kunauwezekano wa kuwepo kwa tishio la kigaidi Jijini
Kampala.
Ubalozi wa Marekani umepata taarifa
za kuwepo kwa uwezekano wa tukio la shambulizi la kigaidi eneo ambalo
raia wa nchi za magharibi wakiwemo wa Marekani hupenda kukaa Jijini
Kampala, na tukio hilo linaweza kufanyika mapema mno.
Ubalozi wa Marekani haujatoa taarifa
zaidi kuhusiana na tukio hilo, lakini nchi ya Uganda ambayo ni rafiki
na Marekani na yenye majeshi yake nchini Somalia ilishashambuliwa
siku za nyuma na wapiganaji wa kundi la Al-Shabaab.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni