.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 26 Machi 2015

MAREKANI YATOA TAHADHARI YA SHAMBULIO LA KIGAIDI NCHINI UGANDA

Ubalozi wa Marekani nchini Uganda umetoa tahadhari ya dharura kwa raia wake nchini Uganda hapo jana inayosema kuwa kunauwezekano wa kuwepo kwa tishio la kigaidi Jijini Kampala.

Ubalozi wa Marekani umepata taarifa za kuwepo kwa uwezekano wa tukio la shambulizi la kigaidi eneo ambalo raia wa nchi za magharibi wakiwemo wa Marekani hupenda kukaa Jijini Kampala, na tukio hilo linaweza kufanyika mapema mno.

Ubalozi wa Marekani haujatoa taarifa zaidi kuhusiana na tukio hilo, lakini nchi ya Uganda ambayo ni rafiki na Marekani na yenye majeshi yake nchini Somalia ilishashambuliwa siku za nyuma na wapiganaji wa kundi la Al-Shabaab.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni