Ndugu na marafiki wa abiria 150
pamoja na watumishi wa ndege Germanwings waliokufa kwenye ajali,
wanatarajiwa kutembelea eneo ilipoanguka ndege hiyo katika milima ya
Alps nchini Ufaransa.
Shirika la ndege la Ujerumani la
Lufthansa litapeleka ndege mbili maalum, moja ikitokea Barcelona na
nyingine ikitokea Duesseldorf hadi Marseille, na baada ya hapo ndugu
hao watasafirishwa kwa njia ya barabara.
Ripoti zimeeleza kuwa mmoja wa
marubani wa ndege hiyo iliyoanguka alikuwa ameondoka katika chumba
cha kuongozea ndege na hakuweza kurejea kusaidiana na mwenzake kabla
ya ndege kuanguka.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni