Balozi wa Saudi Arabia nchini
Marekani amesema Saudi Arabia imeanzisha operesheni ya kijeshi ya
mashambulizi ya anga nchini Yemen dhidi ya waasi wa, Houthi Shia.
Balozi Adel al-Jubeir amesema Saudi
Arabia imefanya hivyo ili kuilinda serikali iliyochaguliwa kihalali
ya rais Abdrabbuh Mansour Hadi.
Waasi hao wanaoungwa mkono na Iran,
wamepata ushindi mkubwa katika miezi ya hivi karibuni, na
kumlazimisha rais Hadi kukimbia mji mkuu wa nchi hiyo Sanaa.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni