Ofisa Habari wa Umoja wa Mataifa Tanzania, Bi. Usia Nkhoma akiwasilisha
mada kwa washiriki wa maadhimisho ya kuwakumbuka waathirika wa utumwa na
biashara zake.
KATIBU Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban
Ki-moon amesema UN itaainisha eneo maalum na la kudumu mahususi kwa
ajili ya kuwakumbuka waathirika wa utumwa na biashara za utumwa
zilizoendeshwa Bahari ya Atlantiki.
Ki-moon
ametoa kauli hiyo kwenye hotuba yake maalum aliyoitoa leo kwenye tukio
la kumbukumbu ya kuwakumbuka waathirika wa utumwa na biashara zake
zilizoendeshwa eneo la Bahari ya Atlantiki.
Alisema
sehemu hiyo maalum ya kumbukumbu itakayokuwa Jijini New York itatoa
fursa kwa watu kutoka mataifa mbalimbali kufika eneo hilo na kujufunza
mengi kupitia matukio yaliajiri nyuma kipindi cha utumwa.
Alisema
kwa taasisi za imataifa ikiwemo UN itatoa fursa kuangalia mikakati yao
katika utendaji wa kazi ili kuhakikisha heshima, uhuru na usawa kwa
binadamu wote vinalindwa sehemu zote.
Alisema
kwa mwaka huu maadhimisho ya kumbukumbu kwa biashara ya utumwa
inawakumbuka zaidi wanawake ambao waliteseka na wengine hadi kuuwawa
kutokana na biashara zautumwa. “…Wanawake wengi walipata mateso makubwa
kutokana na biashara ya utumwa…walinyanyaswa, walitumika kimapenzi na
walilazimishwa kuzaa na hata kuuza watoto wao bila kupenda…,” ilieleza
taarifa ya Ki-moon.
Alisema biashara ya utumwa
bado inaendelea kwa baadhi ya nchi na kutolea mfano kwa mataifa ya Syria
na Iraq ambayo hadi leo maelfu ya wanaume, wanawake na watoto wamekuwa
wakitekwa kuteswa huku vijana na watoto wakinunuliwa na kutumika kwenye
mapigano jambo ambalo ni utumikishaji mbaya.
Kwa
upande wake Ofisa Habari wa Umoja wa Mataifa Tanzania, Bi. Usia Nkhoma
akiwasilisha mada kwa baadhi ya washiriki wa maadhimisho ya kuwakumbuka
waathirika wa utumwa na biashara zake zilizoendeshwa eneo la Bahari ya
Atlantiki, yaliyofanyika Dar es Salaam leo aliikumbusha jamii kujifunza
kupitia historia.
Alisema UN iliamua kutumia
siku ya kumbukumbu kuweza kutoa elimu kwa jamii juu ya masuala anuai
yanayofanywa kinyume na haki za binadamu kumaliza chembe chembe za
utumikiswaji.
Aidha katika maadhimisho hayo
yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Alliance Francais wa jijini Dar es Salaam
washiriki walipata kuona picha za maonesho kuzungumzia biashara ya
watumwa pamoja na filamu anuai.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni