Mabao kutoka kwa Sergio Aguero, Aleksandar Kolarov na Fernandinho yalitosha kuwapa ushindi wa magoli 3-2 timu ya soka ya Manchester City katika mchezo wa ligi kuu nchini Uingereza dhidi ya Aston Villa jana.
Wakicheza katika uwanja wao wa nyumbani wa Etihad, Manchester City iliwachukua dakika tatu za kwanza kuandika bao la kwanza kupitia kwa Aguero.
Kwa ushindi huo, mabingwa hao watetezi ambao hata hivyo nafasi yao ya kuutetea ubingwa msimu huu imepotea, wamefikisha pointi 67 nyuma ya vinara wa ligi hiyo Chelsea wenye pointi 76.
Mabao ya Aston Villa yaliwekwa kimiani na wachezaji Cleverley, Sanchez
Kocha wa Aston Villa Tim Sherwood ( kushoto ) akitoa maelekezo kwa wachezaji wake.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni