.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 27 Mei 2015

MAAFISA WAANDAMIZI WA SHIRIKISHO LA SOKA DUNIANI (FIFA) WAKAMATWA

Maafisa waandamizi wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) pamoja na maafisa wa soko wamekamatwa leo asubuhi na polisi wa nchini Uswizi kufuatia mashtaka ya rushwa yaliyotolewa na Marekani.

Maafisa hao ambao ni sehemu ya vyama wa kimataifa vya soko, wanatarajiwa kurudishwa Marekani baada ya kukamatwa kwenye hoteli moja ya kitalii nchini Uswizi.

Zaidi ya maafisa 10 wa Fifa wanatarajia kufunguliwa mashtaka kwa kuhusika na uhalifu, utakatishaji fedha haramu Jijini New York na Idara ya Sheria ya Marekani.

Mashtaka hayo ni changamoto kubwa kwa Fifa, ambayo rais wake Sepp Blatter anatafuta nafasi ya kuwania muhula wa tano katika uchaguzi utakaofanyika Ijumaa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni