Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, akijumuika na Watoto wa Kijiji cha SOS katika futari maalum aliowaandalia katika makaazi yao Mombasa Zanzibar.
Mkuu wa Utawala wa Kijiji cha SOS Salum A Salum, akizungumza wakati wa hafla hiyo ya futari ilioandaliwa na Mama Mwanamwema Shein
Mkurugenzi wa Kijiji cha SOS Zanzibar Bi Asha Salim Ali, akitowa shukrani kwa Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, wakati wa hafla ya futari aliowaandalia Watoto hao.
Mtoto wa Kijiji cha SOS Mwaamini Makame Msia akitowa neno la shukrani kwa Mke wa Rais wa Zanzibar, Mama Mwanamwema Shein.
Mtoto wa Kijiji cha SOS Lali Amour Haji akisoma dua baada ya hafla ya futari ilioandaliwa na Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa ajili ya Watoto hao, katika makaazi yao.
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Balozi, Mke wa Waziri Mkuu Mama Tunu Pinda na Mama Fatma Karume wakiitikia dua baada ya kumalizika hafla ya futari ilioandaliwa na Mama Mwanamwema Shein.
Watoto wa Kijiji cha SOS Zanzibar wakiitikia dua inayosomwa na Mtoto wa kijiji hicho Lali Amour Haji baada ya kumaliza hafla ya futari ilioandaliwa na Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni