Nyota wa muziki Lovy Longomba kutoka
kundi la Longombaz ambao kwa sasa wapo Marekani, ameendelea kuonyesha
uwezo wake katika jukwaa la muziki la kimataifa, kwa sasa akionekana
kuwa karibu na mwanadada Gwen Stefani, studio kufanya kazi pamoja.
Lovy ambaye amekwishajitengenezea
jina kwa kusuka ngoma ya Change My Life ya Iggy Azalea ambaye ni staa
mkubwa kabisa, kwa nafasi hii mpya ya ukaribu wake na Gwen, tayari
imekwishaonekana kuwa ni nafasi nyingine kubwa ya kuionyesha dunia
uwezo wake.
Huu unakuwa ni mwaka wa 8 sasa kwa
Longombaz tangu kuhama kutoka Kenya, ambapo Lovy ameendelea kufanya
kazi kwa nguvu hasa kwa upande wa utayarishaji muziki, wakati ndugu
yake Christian akijikita katika kutunza familia yake pamoja na
shughuli nyingine.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni