.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 30 Julai 2015

WAHAMIAJI WAANGUSHA UZIO KUWAHI KUPANDA TRENI KUZAMIA UINGEREZA

Mamia ya wahamiaji wameangusha uzio wa fensi kuelekea katika njia ya reli usiku wa jana wakati wakikatiza kujaribu kuwahi kupanda treni kuelekwa Kent katika safari iliyobatizwa jina la kuingia Uingereza ama kifo.

Wabunge waandamizi wa Uingereza wamesema jeshi la Uingereza linapaswa kupelekwa kuwadhibiti wahamiaji hao kwa kuwa inaonekana mamlaka za Ufaransa zimezidiwa na kushindwa kuwazuia.

Hali hiyo imechangia maafisa polisi wa kutuliza ghasia wa Ufaransa 120 kupelekwa katika eneo hilo, ili kusaidiana na askari kanzu 250 walipo katika eneo hilo, hata hivyo idadi hiyo inasemekana haitoshi.
                                          Wahamiaji wanawake wakikatiza juu ya uzio
                                       Mhamiaji akipenya kwenye tundu katika uzio huo

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni