.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 1 Julai 2015

WATU WANNE WAFARIKI DUNIA NA WENGINE 30 KUJERUHIWA BAADA YA TRENI YA MIZIGO KUGONGANA NA BASI LA ABIRIA

Watu 4 wamefariki dunia papo hapo na wengine 30 wamejeruhiwa baada ya treni ya mizigo iliyokuwa ikitokea jijini Dar es Salaam kuelekea jijini Mwanza kugonga basi la abiria lililofahamika kwa jina na Badikadi mkoani Morogoro. 

Taarifa za awali toka kwa mashuhuda na majeruhi wa ajali hiyo wamesema kuwa, ajali hiyo imetokea eneo la njia panda kibaoni katika kijiji cha Kibaoni, kata ya Mpakani. 

Taarifa zaidi zinasema kuwa, dereva wa basi hilo lililokuwa linatoka Kilosa kuelekea Morogoro mjini alitaka kuvuka njia ya treni bila kuwa muangalifu ndipo basi hilo lilipogongwa na treni hiyo ya mizigo. 

Majeruhi wote hivi sasa wanapatiwa matibabu katika Hospitali ya wilaya ya Kilosa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni