.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 24 Novemba 2015

MAADHIMISHO YA SIKU YA TAKWIMU AFRIKA YAFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM

T1
Mgeni Rasmi, Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Prof. Adolf Mkenda akihutubia wadau mbalimbali wa takwimu katika maaadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam ambayo yameongozwa na kauli mbiu ya “Takwimu Bora kwa Maisha Bora”.
T2
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa akitoa maelezo ya utangulizi katika katika maaadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam ambayo yameongozwa na kauli mbiu ya “Takwimu Bora kwa Maisha Bora”
T3
Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia, Habari na Mawasiliano Dkt. Carina Wangwe kutoka Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) akielezea umuhimu wa kujiunga katika Mifuko ya Hifadhi za Jamii wakati wa maaadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam ambayo yameongozwa na kauli mbiu ya “Takwimu Bora kwa Maisha Bora”.
T4
Mkuu wa Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika Prof. Innocent Ngalinda akielezea umuhimu wa takwimu rasmi katika kupanga na kutathmini programu mbalimbali za maendeleo nchini wakati wa maaadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam ambayo yameongozwa na kauli mbiu ya “Takwimu Bora kwa Maisha Bora”.
T5
Baadhi ya wadau mbalimbali wa takwimu wakifuatilia kwa makini matukio yaliyokuwa yakiendelea kwenye maaadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam ambayo yameongozwa na kauli mbiu ya “Takwimu Bora kwa Maisha Bora”.
T6
Mwenyekiti wa Bodi ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu Prof. Milline Mbonile akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa ofisi hiyo pamoja na viongozi wa Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika baada ya kumaliza maaadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam ambayo yameongozwa na kauli mbiu ya “Takwimu Bora kwa Maisha Bora”.

                                                   (PICHA ZOTE NA VERONICA KAZIMOTO).
 

                                                                            Emmanuel Ghula Dar es Salaam

Wizara, Idara, Wakala, Taasisi za Serikali, Mashirika yasiyokuwa ya Serikali na Wadau wa Maendeleo wametakiwa kutumia takwimu zinazotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu katika kupanga na kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo hapa nchini.

Akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika leo jijini Dar es Salaam Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Prof. Adolf Mkenda amesema kuwa matumizi ya takwimu bora ndio msingi katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.
 

“Leo tunasherehekea Siku ya Takwimu Afrika, siku ambayo inatukumbusha umuhimu wa Takwimu katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya taifa letu. Ukiwa na takwimu bora utaweza kutoa huduma zilizo bora,” amesema Prof. Mkenda.
 

Prof. Mkenda amesema uwepo wa takwimu bora zinazoonesha mahitaji halisi ya wananchi ndio dira katika utaoji wa huduma muhimu za kila siku pamoja na upangaji na utekelezaji wa miradi mingine ya maendeleo ya kitaifa.
 

“Maadhimisho haya leo yanazitaka Serikali zetu kuimarisha mifumo ya kitakwimu kwa kuwekeza katika teknolojia ya kisasa ya ukusanyaji, uchambuzi na usambazaji wa Takwimu. Serikali kwa upande wake itahakikisha inaiwezesha Ofisi ya Taifa ya Takwimu kuwekeza katika teknolojia ya kisasa zaidi ili iweze kutekeleza majukumu yake ipasavyo ya ukusanyaji wa Takwimu bora na kwa wakati,” amesisitiza Prof. Mkenda.
 

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dkt. Albina Chuwa amesema Siku ya Takwimu Afrika kwa mwaka huu imelenga katika kuufahamisha umma kuhusu umuhimu wa Takwimu bora kwa maendeleo yao na Taifa kwa ujumla.
 

“Siku hii ya Takwimu Afrika ni muhimu sana kwetu sisi hasa watakwimu kwani tunaitumia kuelimisha umma juu ya umuhimu wa Takwimu katika mustakabali wa maendeleo ya Taifa,” amesema Dkt. Chuwa.
 

Dkt. Chuwa amesema kupitia maadhimisho haya yanayoongozwa na kauli mbiu ya “Takwimu Bora kwa Maisha Bora”, itawasaidia wananchi kutambua kuwa uwepo wa takwimu bora ndio njia ya upatikanaji wa maendeleo stahiki.
 

Nae Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kutoka Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Dkt. Carina Wangwe amesema wakiwa kama watumiaji wakubwa wa 
Takwimu zinazotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu katika utekelezaji wa majukumu yao ndio wanathamini mchango wa takwimu rasmi katika kupanga mipango ya maendeleo.
 

“Sisi ni wadau wakubwa na watumiaji wa takwimu zinazotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu, leo hii tupo hapa ili kushirikiana na ofisi hii ili kuhakikisha teknolojia ya kisasa inatumika katika uboreshaji wa Takwimu na kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma mbalimbali kwa jamii,’ amesema Dkt. Wangwe.
 

Siku ya Takwimu Afrika huadhimishwa tarehe 18 Novemba, kila mwaka, Kwa hapa Tanzania maadhimisho haya yamefanyika Novemba 23, 2015 ambapo kauli mbiu ya maadhimisho hayo kwa mwaka huu ni “Takwimu Bora kwa Maisha Bora”.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni