Mbunge mmoja wa Japan ambaye aliibua
mjadala mkali bungeni wa likizo ya uzazi kwa wanaume, amejiuzulu
ubunge baada ya kukiri alichepuka wakati mkewe akitarajiwa
kujifungua.
Mbunge huyo Kensuke Miyazaki ameomba
msamaha katika mkutano na waandhishi wa habari, kwa kusababisha
kuibuka kwa hasira za umma kuhusiana na kuisaliti ndoa yake.
Bw. Miyazaki aliibua mjadala mwezi
uliopita baada ya kuwa mbunge wa kwanza mwanaume Japan kuomba likizo
ya uzazi.
Mbunge Kensuke Miyazaki akiinama ikiwa ni ishara ya kuomba msamaha
Mbunge Kensuke Miyazaki akiinama ikiwa ni ishara ya kuomba msamaha
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni