Wawania urais wa Democratic Hillary
Clinton na Bernie Sanders wamechuana kuhusiana na kumuunga mkono rais
Barack Obama katika mdahalo wao wa kwanza tangu kura za maoni za New
Hampshire.
Bi. Clinton aliamua kujitanabaisha
kama mtetezi wa utawala wa rais Barack Obama, alimshambulia vikali
Bw. Sanders kwa kumkosoa rais.
Bi. Clinton alisema aina ya ukosoaji
anayosikia kwa Bw. Sanders ilitarajiwa kufanywa na wapinzania wao wa
chama cha Republicans.
Majimbo ya Nevada na South Carolina,
yenye idadi ndogo ya watu yatafuatia katika kura za maoni.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni